Ufyatulianaji mkali wa risasi
umetokea kaskazini mwa Paris katika mtaa wa Saint Denis na ripoti
zinasema operesheni ya polisi kuhusiana na mashambulio ya Ijumaa
inaendelea.
Maafisa kadha wa polisi wamejruhiwa, kituo cha runinga cha BFMTV cha Ufaransa kimeripoti.
Video
iliyoonyeshwa na vituo vya televisheni vya BFMTV na iTele zimeonyesha
watu walioshuhudia wakisema milio ya risasi ilianza kusikika saa kumi
unusu alfajiri saa za Ufaransa.
Naibu meya Stephane Peu amewahimiza raia wasalie manyumbani, akisema "hili si shambulio jipya bali ni operesheni ya polisi".
Awali,
duru za kiusalama zilisema video ya kiusalama ilikuwa imeonyesha huenda
kulikuwa na mshambuliaji wa tisa mashambulio hayo ya Ijumaa.
Watu 129 walifariki kwenye mashambulio yaliyotokea maeneo sita mjini Paris.
Kundi la Islamic State (IS) limesema ndilo lililotekeleza mashambulio hayo.
Ripoti moja inasema barabara zimefungwa eneo la Place Jean Jaures mtaa wa Saint Denis.



0 comments:
Post a Comment