![]() |
| south carolina |
Polisi katika jimbo la South
Carolina nchini Marekani wamesema kuwa mtu mmoja aliyejihami kwa bunduki
amewapiga risasi na kuwaua watu tisa ndani ya kanisa la kimethodist.
Polisi
wa eneo hilo la Charleston wameelezea kuwa kwa sasa
wanamtafuta
mshukiwa huyo anayeaminiwa kuwa kijana wa kizungu katika miaka ya
ishirini.
Shambulio hilo limefanyika ndani ya kanisa la Emmanuel
African Methodist Church, kanisa linaloaminiwa kuwa la zamani zaidi la
kiafrika nchini Marekani
Polisi wamesema kuwa shambulio hili ni la chuki ya rangi ya ngozi.


0 comments:
Post a Comment